JULAI
3 KIKOSI cha Mabingwa Manchester United kitakusanyika tena ndani ya
Carrington, Kituo cha Mazoezi yao Jijini Manchester, na pengine Straika
Wayne Rooney atakuwepo licha ya uvumi mzito wa yeye kuhama.
Lakini, mwenyewe Rooney pamoja na kambi
yake ya Washauri, imekataa kabisa kuwa Mchezaji huyo hakuwa na nia ya
kuihama Manchester United.
Hadi hii leo si Rooney wala Msemaji wake yeyote alietamka kinagaubaga kuwa Staa huyo anataka kuipa teke Old Trafford.
Mwezi Oktoba 2010, Wayne Rooney aliwahi
kuitaka Man United imruhusu kuhama lakini, baada ya majadiliano na
makubaliano ya haraka haraka, akaongezewa Mshahara na kufikia Pauni
250,000 kwa Wiki na kupewa Mkataba mpya wa Miaka mitano.
Wakati huo, wakati hali ikiwa tete,
Kundi la Mashabiki wa Man United walizingira Nyumba yake na kumpa
vitisho na Siku ya pili yake tu Man United ikatamka Rooney anasaini
Mkataba mpya.
Mara baada ya Sir Alex Ferguson kudokeza
kuwa Rooney anataka kuhama, Man United, kama Klabu, ilitoa tamko rasmi
kuwa Mchezaji huyo, ambae Mkataba wake unamalizika Mwaka 2015, hauzwi.
Tamko hilo lilifuatia kuibuka kwa
shamrashamra za Klabu mbalimbali kutaka kumsaini ikiwemo hata Arsenal
ambayo haisifiki kwa kununua Wachezaji wa ‘Bei kubwa’
Sasa Sir Alex Ferguson hayuko tena
kwenye picha na Meneja mpya ni David Moyes ambae ndio Mtu alieibua
kipaji cha Wayne Rooney wakati wakiwa nae Everton kwa kumpa nafasi
kucheza Timu ya Kwanza akiwa na Miaka 16 tu.
0 comments:
Post a Comment