STRAIKA wa Newcastle Papiss Cisse yupo
kwenye hali ngumu ya kuvaa Jezi ya Klabu yake Newcastle ambayo sasa
Mdhamini wake ni Kampuni ya Mikopo kitu ambacho ni kinyume na imani yake
ya Kiroho.
Cisse:
-UMRI: 28
-UTAIFA: Senegal
-KLABU: Douanes Dakar, Metz, Freiburg & Newcastle
-NEWCASTLE MAGOLI: 26
Msimamo huo pia umedakwa na Chama cha
Wachezaji wa Kulipwa huko Uingereza, PFA, Professional Footballers'
Association, na Makamu Mkuu wake, Bobby Barnes, amesema hiyo ni hali
ngumu lakini anatumaini Klabu ya Cisse itamsaidia.
Cisse alijiunga na Newcastle Januari 2012.
Tatizo kama la Cisse lilimkumba Straika
wa Mali Frederic Kanoute wakati akichezea Klabu ya Spain Sevilla Mwaka
2007 wakati Klabu hiyo ilipoingia Mkataba na Kampuni ya Uchezeshaji
Kamari wakati Kanoute ni Mwislam.
Imani za Kiislamu zinakataza kabisa Kamari na Kanoute ilibidi acheze huku nembo ya Kampuni hiyo ikiwa imezibwa.
0 comments:
Post a Comment