Wednesday, October 16, 2013

INASIKITISHA! MTOTO WA MIAKA NANE ASONGA UGALI IKWA NI BAADA YA KUTELEKEZWA NA WAZAZI WAO TAZAMA PICHA ZAIDI YA 6 ZA WATOTO HAWA WANAVOTESEKA!!!!


“Baba ameondoka tangu Mei (mwaka huu) na kwenda Umalila, Mbeya Vijijini ambako inasemekana ameoa mwanamke mwingine,” alisema Agustino......................................

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, watoto wawili wa kike na kiume wanaoishi katika Mtaa wa Jacaranda, Airport jijini Mbeya, wenye umri wa miaka 7 na 8 wametelekezwa na wazazi wao kwa muda wa miezi mitano bila ya kupata huduma kutoka kwa wazazi wao.

Wazazi hao ambao majina yao hayakupatikana, wamewaacha watoto hao, Agustino Steven (8) na Rebeca Steven (7) wanaosoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Mapambano iliyopo Kata ya Iyela jijini hapa na kwenda kuolewa na kuoa mbele ya safari.
Mbaya zaidi, watoto hao wameachwa katika nyumba ya kupanga wakati wakiwa na umri ambao hawawezi kulipa kodi ya nyumba, hivyo kuishi kwa busara za mwenye nyumba hiyo.
“Baba ameondoka tangu Mei (mwaka huu) na kwenda Umalila, Mbeya Vijijini ambako inasemekana ameoa mwanamke mwingine,” alisema Agustino.
Mtoto huyo aliendelea kudai kwamba baada ya muda, mama yao naye aliondoka kwenda Mbozi ambako inasadikika kuwa ameolewa na mwanaume mwingine.
Hata hivyo, pamoja na kuishi katika nyumba hiyo, watoto hao hawakuwa na budi kujitafutia riziki kwa kuzoa takataka kutoka kwenye nyumba za majirani na kuzipeleka majalalani kwa ujira wa kati ya shilingi 200 na 500.
Baada ya kuulizwa kwa nini wanafanya kazi hiyo, ndipo Agustino na Rebeca walipofunguka na kutoa simulizi ya kusikitisha kwa kudai kwamba walikuwa wakijitahidi kutafuta fedha angalau wawe wanakula mlo mmoja kwa siku.
“Mara nyingi asubuhi huwa tunaenda shule bila kunywa chai, hela tunazozipata kwa kuzoa takataka zinatusaidia kununua unga na mboga na kujipikia mlo wa usiku,” alisema Rebeca.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mwenyekiti wa Dawati la Jinsia lililopo chini ya Jeshi la Polisi, Mary Gumbo amesema baada ya kupata taarifa hizo alifika eneo la tukio na kuwahoji watoto hao.
Mwenyekiti huyo amewaomba majirani na wananchi kuwasaidia polisi ili kuweza kuwabaini wazazi wa watoto hao sehemu walipo ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
“Majirani wanatakiwa kuwahudumia watoto hao mpaka wazazi wao watakapopatikana na kuhakikisha wanaendelea na masomo kama kawaida,” alisema Gumbo.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wetu, umebaini kwamba wazazi hao waliwahi kumwacha binti yao mwenye umri wa miaka 17 aliyefahamika kwa jina la Salome Steven kwa kutompeleka shule na kumpa jukumu la kuwalea wadogo zake hao.
Kutokana na ugumu wa maisha na harakati za kutafuta fedha kwa ajili ya wadogo zake, binti huyo aliishia kupachikwa mimba na kuwakimbia wadogo zake, akaenda kuishi kwa rafiki yake.
Posted by http://thesuperonenews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment