Friday, January 17, 2014

Kichaa cha Mbwa: Wakazi Dodoma Waathirika


Aghalabu siku haiwezi kwisha bila kuona mbwa akikatisha katika mitaa ya katikati ya mji, wakati wa mchana bila kuwa chini ya uangalizi. 0
Mbwa ni mnyama wa kufugwa mwenye manufaa chekwa. Anaisaidia jamii kwa mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi, kazi za kiusalama na  hata utunzaji wa mazingira.
Kwa sababu anaishi kwa ukaribu kabisa na wanajamii anahitaji kutunzwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanapata chanjo.
Hali katika Mkoa wa Dodoma, imekuwa kinyume kwa sababu kumekuwa na idadi kubwa ya  mbwa wanaozurura mitaani jambo ambalo linahatarisha maisha ya wakazi.
Uchunguzi uliofanywa katika maeneo mbalimbali ulibaini kuwa kuna idadi kubwa ya mbwa wanaozurura ovyo kwenye maeneo ya Area A, Swaswa, Area D na hata katikati ya mji.
Aghalabu siku haiwezi kwisha bila kuona mbwa akikatisha katika mitaa ya katikati ya mji, wakati wa mchana bila kuwa chini ya uangalizi.
Ofisa Mfuatiliaji wa Mgonjwa yanayotokana na chanjo mkoni hapa, Paul Mgeni, anasema tatizo la watu kung’atwa na mbwa ni kubwa.
“Si chini ya watu 10 ambao wamekuwa wakiripoti katika hospitali yetu (Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma) kuwa wameumwa na mbwa na hasa hasa wanaoathirika ni watoto wadogo,” anasema.
Takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha kati ya Januari na Oktoba mwaka jana, jumla ya watoto  278 walio chini ya umri wa miaka mitano waling’atwa na mbwa mkoani hapa.
Kati ya hao watoto 165 walikuwa ni wa kiume wakati watoto 113 walikuwa ni wa kike. Kwa mujibu wa takwimu hizo watu zaidi ya umri wa miaka mitano waliong’atwa na mbwa katika kipindi hicho, walikuwa ni 1580 ambapo kati ya hao wanaume walikuwa 931 wakati wanawake walikuwa 649.
Mwaka juzi, watoto chini ya miaka mitano walikuwa ni 326 na waliojuu ya miaka mitano walikuwa ni 877.
Mageni anasema watu 16 walipoteza maisha mkoani hapa kwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.
Hata hivyo anasema wengi wa watu wanaokuja kupata matibabu hawana uwezo wa kumudu gharama za kununua  chanjo.posted by http://thesuperonenews.blogspot.com/

0 comments:

Post a Comment