Tuesday, October 15, 2013

fahamu Kanuni bora 10 za usalama wa kompyuta yako


Cha msingi ni kufuata tu kanuni, kwani kwa kufanya hivyo unaweza kwa kiasi kikubwa kuepukana na mambo mengi yanayoweza kuhatarisha usalama wa kompyuta yako kama vile athari za virusi.Ingawa mara nyingi husemwa kuwa hakuna usalama wa asilimia mia moja kwenye ulimwengu wa teknolojia ya kompyuta, ila kinga ni bora kuliko tiba.
Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wanatumia kiasi kikubwa cha fedha kuimarisha ulinzi katika maeneo yao ya makazi?
Ndivyo ilivyo, tembelea hata katika makazi ya watu wa kawaida, madirisha yamejaa nondo, nyumba zimezungukwa na kuta ndefundefu. Wengine wamefikia hatua ya kufuga mbwa kwa ajili ya kuwalinda.
Nimeanza kwa kutoa mifano hii kuonyesha umuhimu wa kuzilinda kompyuta zetu. Ingawa mara nyingi husikika ikisemwa kuwa hakuna usalama wa asilimia mia moja kwenye ulimwengu wa teknolojia ya kompyuta, ila kinga ni bora kuliko tiba.
Cha msingi ni kufuata tu kanuni, kwani kwa kufanya hivyo unaweza kwa kiasi kikubwa kuepukana na mambo mengi yanayoweza kuhatarisha usalama wa kompyuta yako kama vile athari za virusi.
Makala haya yanataja baadhi ya kanuni za msingi unazopaswa kufuata ili kutunza usalama wa kompyuta yako.
 Tumia programu unazozihitaji
Watumiaji wengi wa kompyuta tumekuwa waathirika wa matatizo ya kompyuta zetu ama kwa kujua au kwa kutokujua. Kwanza ieleweke kuwa kompyuta nyingi zimekuwa zikiathiriwa  kiusalama kwa makosa yaliyomo kwenye kompyuta husika.
Hizi ni zile kompyuta zenye programu ambazo hazijaandikwa kiusahihi. Tuchukue  mfano wa nyumba inayovuja, kwa kuwa tu paa lake halikuezekwa ipasavyo. Au ukuta wa nyumba unavyoweza kuanguka, kwa kuwa haukutengenezwa kwa kufuata taratibu za ujenzi.
Kama kompyuta yako ina programu ambayo haikuandikwa kwa usahihi, matatizo mengi hutokea yanayoweza kuhatarisha kifaa hicho. Programu hizi sio tu zitahitilafiana na mtambo endeshi (OS) wa kompyuta yako, pia zinaweza kutoa mianya kwa  wavamizi kuingia kwenye kompyuta yako  kupitia kwenye mianya iliyopo kwenye  programu hizi.
Cha kufanya: Mosi, ondoa programu usizotumia. Tuache tabia ya kuweka programu nyingi katika kompyuta zetu ambazo kwa hali ilivyo hatuzitumii kabisa. Kwa kawaida programu hujaza nafasi, kuweka uchafu na hatimaye kuiweka kompyuta matatani.
Kumbuka unapoweka (install) baadhi ya programu katika kompyuta yako, nazo huweka programu nyingine zinazoambatana nazo bila ya wewe kujua. Hatimaye unajikuta umelundika lundo la programu.Posted byhttp://thesuperonenews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment