Tuesday, December 3, 2013

Je wajua ? kuwa Wenye virusi vya ukimwi (VVU) wabaininika!

Wanawake katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wanaongoza kwa maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) ukilinganisha na wanaume, imeelezwa hapa chini............................

Sababu kubwa zinazoelezwa kuchangia hali hiyo ni mwendelezo wa mila potofu, ndoa za jinsia moja, kurithi wajane, ndoa za wake wengi, ukeketaji, kuachana wanandoa na umaskini wa kipato.
Akisoma risala Siku ya Ukimwi Duniani, Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Nyakarima, Juma Wilson alisema takwimu za 2010-2011 zinaonyesha kuwa wanawake 261 walikutwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, wakati wanaume walikuwa 170.
Mwaka 2011-2012, wanawake 251 waligundulika na virusi, wakati wanaume walikuwa 133. mwaka 2012-2013 wanawake wenye virusi walikuwa 170, wanaume 61.
Aidha, katika kampeni ya kuhamasisha watu kupima virusi katika Wilaya ya Tarime kati ya Novemba 21 na Desemba 1, imebainika wanawake wanaongoza kwa maambukizi. Katibu wa Afya Hospitali ya Wilaya Tarime, Sufiani Mageta alisema katika kampeni ya kupima kwa hiari watu 6355, kati ya hao wanawake 44 na wanaume 24 walikutwa na maambukizi ya virusi.
Aidha akifafanua, Mageta alisema watumishi wa Kampuni ya North Mara 1,320 waliopima kwa hiari, 30 walikutwa na maambukizi ingawa kwa mwaka huu maambukizi yamepungua kwa asilimia 2.2 kulinganisha na mwaka jana.
Katibu Tarafa ya Inchage Machango Jonathani aliyekuwa mgeni rasmi katika kilele cha Siku ya Ukimwi, ameitaka jamii kuachana na mila potofu zinazochangia kuongezeka kwa maambukizi.
posted by http://thesuperonenews.blogspot.com/

0 comments:

Post a Comment