Monday, June 2, 2014

TAZAMA:MSHAMBULIAJI Samuel Eto's alichokifanya jana baada ya kuifungia cameroon na kumbusha morinho kwa kwa vitendo alichokizungumza kipind cha nyuma

MSHAMBULIAJI Samuel Eto's jana amerudia kushangilia kama kikongwe baada ya kuifungia Cameroon bao la kuongoza ikitoka safe ya 2-2 na Ujerumani katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Kombe la Dunia.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 33 alimtoka beki Mats Hummels kuuwahi mpira kabla ya kumtungua kioa wa Ujerumani, Roman Weidenfeller dakika ya 62.

Eto'o, alishangilia kama hivyo awali katika klabu yake Chelsea baada ya kufunga dhidi ya Manchester United katika Ligi Kuu ya England, kujibu mapigo ya kocha wake, Mreno Jose Mourinho aliyehoji umri wake akidai ni mkubwa kuliko miaka anayotaja. Bao lingine la Cameroon lilifungwa na Choupo-Moting dakika ya 78, wakati mabao ya Ujerumani yalifungwa na Muller dakika ya 66 na Schurrie dakika ya 71. 
Kikosi cha Ujerumani kilikuwa: Weidenfeller, Boateng, Mertesacker, Hummels, Durm/Howedes, dk85, Khedira/Kramer, dk73, Kroos, Muller, Ozil/Podolski, dk63, Reus, Gotze/Schurrle, dk58. 
Cameroon: Itandje, Djeugoue, Bedimo/Assou-Ekotto, dk58, N'Koulou, Song, Mbia/N'Guemo, dk46, Enoh, Matip, Choupo-Moting, Moukandjo, Eto'o/Webo, dk90.
Opener: Samuel Eto'o pokes the ball home to give Cameroon the lead against Germany on Sunday night
La kwanza: Samuel Eto'o akifunga bao la kwanza la Cameroon katika safe ya 2-2 na Ujerumani jana

0 comments:

Post a Comment