Friday, October 25, 2013

WENGER ‘AOTA’ FERGIE KURUDI, PELLEGRINI ADHARAU VIJEMBE VYA MOURINHO

FERGIE_n_WENGER-KICHEKO
Arsene Wenger amekiri hatastushwa ikiwa Sir Alex Fergusonatabadilika na kurudi tena kwenye Soka ndani ya Miezi 6 tangu astaafu Umeneja Manchester United.



>>PELLEGRINI: ‘SIMJUI YEYE! ALIFANYA KAZI SPAIN NA MIMI NILIKUWA KLABU NYINGINE!’
WAKATI Arsene Wenger akisema hatashangaa ikiwa Sir Alex Ferguson atarudi tena kuongoza kwenye Soka, Manuel Pellegrini amekataa kujitumbukiza kwenye kupigana vijembe na Jose Mourinho huku Timu zao, Chelsea na Manchester City, zikitarajiwa kucheza Jumapili kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
SOMA ZAIDI:
WENGER: ‘SIR ALEX FERGUSON ANAWEZA KURUDI!’
Ingawa Sir Alex Ferguson amesisitiza hatarudi tena kufundisha Soka lakini Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, ana wasiwasi na ametamka: “Baada Miezi 6 tutajua wazi kuhusu hili. Huwezi kuondoka moja kwa moja. Ni kama kutumia Dawa kwa Miaka 30 na ghafla kuacha!”
Maneno hayo ya Wenger yamekuja kwenye Wiki ambayo Sir Alex Ferguson amezindua Kitabu chake, ‘Sir Alex Ferguson-My Autobiography’,  ambacho ndani yake ipo Sura nzima, iitwayo ‘Kushindana na Wenger’.
Akikiri kuwa hajasoma Kitabu hicho, Wenger amesema: “Inaelekea Ferguson alikuwa akitayarisha Kitabu chake wakati bado ni Meneja. Nadhani kila Usiku alikuwa akikaa na kuandika!”
PELLEGRINI AMDHARAU ‘MBWABWAJAJI’ MOURINHO!
PELLEGRINI-KIDOLEMeneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amegomaMOURINHO_V_REFAkuburuzwa na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho na kuingizwa kwenye malumbano wakati Timu zao zikijitayarisha kupambana kwenye Mechi ya Ligi Kuu England huko Stamford Bridge hapo Jumapili.
Pellegrini na Mourinho wanayo historia yao tangu huko Spain ambapo Mourinho alimbadili Pellegrini kuwa Meneja wa Real Madrid baada ya Pellegrini kumaliza Msimu akiwa Nafasi ya Pili nyuma ya Barcelona.
Na Mourinho amebatuka: “Nafasi ya Pili ni Timu ya Kwanza kufungwa. Kama Real wangenifukuza mimi, nisingekwenda Malaga! Ningekwenda kwenye Timu kubwa huko Italy au England!”
Lakini, licha ya kupigwa kijembe, Pellegrini amekataa kuburuzwa kwenye malumbano wakati akijitayarisha kukutana uso kwa uso na Mourinho kwa mara ya kwanza Nchini England.
Pellegrini amesema: “Huwa sijiingizi kwenye malumbano na stajiingiza sasa!”
Aliongeza: “Simjui yeye. Alifanya kazi Spain, na mimi nilikuwa Klabu nyingine. Tulicheza Real na Malaga. Hamna la zaidi, sina malalamiko na yeye!”
BPL: LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Oktoba 26
1445 Crystal Palace v Arsenal
1700 Aston Villa v Everton
1700 Liverpool v West Brom
1700 Man United v Stoke
1700 Norwich v Cardiff
1930 Southampton v Fulham
Jumapili Oktoba 27
1630 Sunderland v Newcastle
1900 Chelsea v Man City
1900 Swansea v West Ham
1900 Tottenham v Hull
**KUANZIA JUMAPILI, MAJIRA HUKO ENGLAND YANABADILIKA.
-MECHI ZITAANZA KUCHEZWA SAA 1 MBELE YA TILIVYOZOEA BONGO
-TOFAUTI YA MASAA ITAKUWA NI MATATU [BONGO WATAKUWA SAA 3 MBELE] 

0 comments:

Post a Comment