Thursday, June 20, 2013

WAANGALIE XAVI NA ANDRES INIESTA WAPYA HAPAHAPA


Ingawa kuna mvuto mkubwa wa uimara na ubora wa kikosi cha sasa cha mabingwa wa dunia na ulaya, msingi mkuu wa mafanikio ya Spain katika miaka ya hivi karibuni yametokana na kuwa na wachezaji imara wanaounda nafasi ya kiungo ya timu hiyo Sergio Busquets, Xabi Alonso, Xavi na Andres Iniesta.  

Huku Busquets kwa utaratibu kabisa akiwa anaulinda ukuta wa nyuma, Alonso kwa pembeni akitoa msaada pamoja na kupiga pasi ndefu ndani ya dimba lote, Xavi akiwa daraja baina ya kiungo na safu ya ushambuliaji, na Iniesta akifanya maajabu yake kuelekea ndani ya eneo la penati, wachezaji hawa wanne wameshacheza jumla ya mechi 369 za kimataifa, wakijenga msingi mzuri na imara wa mafanikio ya Spain. 

Habari kwa Spain 'La Roja' (na habari nzuri kwa timu nyingine duniani) ni kwamba wachezaji watatu kwenye kundi hil- Alonso (miaka 31), Xavi (33) na Iniesta (29) - wanaweza wakawa wanaelekea ukingoni wa maisha yao ya soka la kiwango cha juu - labda kwenye Kombe la Dunia mwakani. Timu hii ya sasa inaelekea kwenye mwisho wake wa zama za mafanikio.  
 
Ingawa, uwezo ulionyeshwa na kikosi cha timu ya taifa ya Spain chini ya umri wa miaka 21 - ambao wametwaa ubingwa wa Euro hivi karibuni kwa kuitandika Italia 4-2 - inaonekana wazi kwamba wabadala halisi wa kikosi cha sasa cha wakubwa cha Spain wapo tayari kuiteka dunia. Spain U21 nayo imeundwa juu ya msingi wa viungo watatu ambao wana sifa zenye kufanana na viungo wa kikosi cha wakubwa. 

 
Hwafanani kwa sifa zote na akina XAVI - hakuna anayeweza kuwa sawa nao - lakini wachezaji hawa watatu vijana wana nafasi ya kuja kuwa mastaa wakubwa kwa namna yao.

Wachezaji hawa ni Asier Illarramendi, Thiago Alcantara na Isco.


THE NEW XABI ALONSO: ASIER ILLARRAMENDI

Mtulivu, anayejua kuuchezea mpira - kiungo ambaye alianza maisha yake ya soka kwenye klabu ya Real Sociedad, alianza kujulikana wakati timu yake ikisaka nafasi ya kufuzu Champions League. 

Maneno haya yanaweza kutumika katika kumuelezea Xabi Alonso, ambaye soka lake liliibukia wakati Real Sociedad walipokuwa washindi wa pili wa La Liga kwenye msimu wa 2002-03 kabla ya kuondoka na kuelekea Liverpool, na Illarramendi, kiungo huyu ambaye alikuwa nyuma ya mafanikio ya Sociaedad katika kushika nafasi ya nne katika La Liga msimu uliopita.

Illarramendi ni mmoja ya mashujaa wasiotajwa sana kwenye kikosi cha U21 cha Spain kilichofanya balaa huko Israel, lakini wachambuzi wengi waliona namna alivyokuwa na umhimu ndani ya timu hiyo, na ndio maana sikushangazwa kuona klabu kama Arsenal wakihusishwa na kuiwinda saini ya mhispania.


Kama Alonso, kijana huyu ndio moyo mkuu wa timu, akicheza mbele watu wanne wa nyuma akilazimisha flow na kasi ya mchezo kwa pasi nzuri zenye maana.

Nidhamu yake ya kutokuwa mbinafsi - akijiweka nafasi ya kuulinda timu na kuwapa uhuru washambuliaji kucheza kwa uhuru, na moja ya mechi zake nyingi za kimataifa kwenye timu ya wakubwa ipo njiani. 

THE NEW XAVI: THIAGO ALCANTARA

Kiungo huyo wa Barcelona Thiago anatokea kwenye familia inayokula na kulala kupitia soka: baba yake Mazinho alikuwa mwanasoka wa kimataifa wa Brazil ambaye alikuwemo kwenye kikosi kilichoshinda World Cup 1994 wakati mdogo wake Rafael - maarufu kama Rafinha - ni zao lingine la academy ya Barcelona ambaye tayari ameshaanza kupata nafasi kwenye timu ya kwanza ya Barca.
Thiago alizaliwa nchini Italia wakati baba yake akiichezea Lecce, baadae akaenda kuishi Brazil na baadae akahamia Spain akiwa bado mtoto mdogo, akaanza kujifunza soka kwenye academy ya Barca kabla ya kuanza kupata nafasi katika kikosi cha kwanza akiwa na umri wa miaka 18. 
Akiwa nahodha aliiongoza Spain Under-21 wakati wa michuano ya Euro iliyoisha hivi karibuni, akitengeneza vichwa vya habari baada ya kuifungia timu yake hat trick kwenye fainali ya ushindi wa 4-2 dhidi ya Itali. s

Kiwango cha mechi hiyo kilileta kidogo mkanganyiko kwa sababu kufunga sio kawaida ya Thiago - amewahi kufunga mabao mawili katika mechi za timu za wakubwa - achana na hat trick. 


Lakini kijana huyu mwenye miaka 21 ni fundi haswa, akiwa na 'first touch' nzuri sana, anajua kuuchezea mpira, mpiga pasi nzuri sana kiasi kwamba watu wengi ndani ya Camp Nou wamekuwa wakimuona kama mrithi halisi wa wa Xavi. 

Ingawa, Thiago ameanza kuchoshwa na kutopata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Barca na kushindwa kwake kucheza japo asilimia 60 za mechi za msimu uliopita kunamaanisha kipengele chake cha bei ya kuuvunja mkataba wake na Barca kimeshuka kutoka 90m Euros mpaka 18m. 
Manchester United na Bayern Munichni moja kati kadhaa zinazotajwa kuwania saini yake wakati media za Catalan media zimeanza kampeni ya kumfanya ashawishike kubaki. 

Hata mtu ambaye ndio anayempigisha benchi kwenye kikosi cha kwanza, gwiji  Xavi, amemshauri kinda huyo kuendelea kubaki Camp Nou: "Thiago ni mchezaji wa aina yake. Sio tu mchezaji ambaye anasubiri aje kucheza huko mbele bali hata sasa anaweza kucheza.

"Ningependa kumshauri Thiago abaki na kuwa mvumilivu kwa sababu atapata mafanikio akiwa hapa Barca."


Kwa bahati ushauri wote huu wa Barcelona, utaangukia kwenye sikio la kiziwi, huku Thiago akitegemewa kufanya uamuzi wake wa kuondoka Barcelona hivi karibuni - Manchester United ndio anapotakiwa zaidi.

  ANDRES INIESTA MPYA: ISCO

Mshindi wa tuzo ya bora kinda barani ulaya mwaka 2012; mshindi wa Mchezaji bora chipukizi wa wa La Liga msimu wa 2011-12; mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mashindano ya Euro U21 mwaka 2013.... Francisco Roman Alarcon Suarez ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa mno.
Isco ni shabiki mkubwa wa klabu ya Barcelona na ana mbwa mdogo ambaye amempa jina la Messi, lakini wakati anakuwa amekuwa akimuhusudu sana Andres Iniesta - na hilo linaonekana. 

Kama ilivyo kwa shujaa wake, star huyu wa Malaga ni mmoja ya wachezaji wanaojua sana kukokota mpira ambaye ana balance nzuri na anaweza kupita katikati ya mabeki kwa kasi mno akitokea winga ya kushoto - pia anajua kupiga pasi za mwisho pamoja na kupiga mashuti.  
Jambo la kutisha zaidi, eneo moja ambalo ana ubora kumzidi Iniesta ni kwenye ufungaji. Alifunga mabao 17 kwa klabu yake na nchi yake msimu uliopita, yakiwemo matatu aliyoifungia Malaga na kusaidia kwenda robo fainali ya klabu bingwa ya ulaya.

Kipaji chake ni kikubwa kiasi kwamba Malaga wamemuakea kais cha 35m Euros kwa timu yoyote inayotaka kumnunua, huku  Manchester City na Real Madrid wakiwa wanaongoza mbio za kushinda saini yake. in

 
Mapema wiki hii, Isco alikiri kwamba ana ofa mbili kutoka kwenye klabu kubwa barani ulaya na hatma yake itaamuriwa mwishoni mwa mwezi huu, huku kukiwa na mategemeo ataamua kumfuata kocha wake wa zamani
Manuel Pellegrini Etihad Stadium. Ikiwa hilo litatokea basi mashabiki wa City wakae tayari kwa burudani ya aina yake.

Wakati Illarramendi, Thiago na Isco wakiwa tayari kujiunga na David De Gea kwenda kwenye vilabu vikubwa na kupata nafasi - ni wazi kwamba supply ya vipaji ya Spain haionyeshi dalili zozote za kupungua.

Na haishii hapo tu: Fifa Under-20 World Cup inaanza hivi karibuni huko Uturuki na timu ya Spain inapewa nafasi kubwa ya kubeba ubingwa huo.

0 comments:

Post a Comment