Tuesday, June 18, 2013

Mkoani Arusha hali sio shwari!!!!



.Arusha.
 Katika mkusanyiko huo kuna Askari Polisi mmoja ambae alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa kwa mabomu na kufariki June 15 2013 na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa.

Baada ya hapo hawa Wafuasi hawakupenda kitendo cha Polisi kujichanganya nao hivyo ikazuka kama kutoelewana huku wakitaka atoke, baada ya dakika kadhaa huku pia Viongozi wa Chadema wakihutubia…. ndio mabomu yakaanza kusikika.

Lakini pia “Baada ya Tundu Lissu wa Chadema kuhutubia na kusema chanzo cha vifo vya June 15 2013 ni Polisi, yani vifo hivyo viliratibiwa na RPC Arusha… mabomu ya machozi ndio yakaanza kulipuliwa”
 
Mpaka mida ya saa kumi na moja wafuasi wa Chadema bado wako maeneo ya Soweto Arusha, wamegoma kuondoka na kusema wanataka kujua kwanza usalama wa Viongozi wao…. lakini pia mabomu yanaendelea kusikika kwenye sehemu nyingine kama Sanawari, Arusha mjini, Mianzini na maeneo mengine.www.Thesuperonenews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment