Friday, January 24, 2014

SAIKOLOJIA&UTAFITI: Tatizo la wanaume dhaifu linavyohatarisha ndoa


Ni vigumu kufahamu haya, lakini ndio ukweli kuwa kuna kasi ya kuongezeka kwa wanaume dhaifu nchini na ulimwengu kwa ujumla.kama .......................
Kulingana na taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO), tatizo hili la wanaume dhaifu linaongezeka kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kuendekeza ulevi, matumizi ya tumbaku/sigara, kutokula kwa kuzingatia mchanganyiko wa vyakula (ulaji usiofaa) na watu kutopenda mazoezi.
Hapa nchini hakuna utafiti thabiti uliofanywa lakini nafikiri tutakubaliana kuwa tatizo hili lipo tena ni kubwa, kwani kinyume na hilo kusingekuwa na watu wengi wanaojitangaza kwamba wanatibu. Marekani  wamefanya utafiti, Shirika liitwalo National Ambulatory Medical Care Survey (NAMCS) ambalo linasifika kwa kufanya tafiti mbalimbali za masuala ya afya, linasema kwamba ukionana na Wamarekani 1,000 ujue kwamba 22 ni wanaume dhaifu.
NAMCS ikasema pia kwamba zaidi ya wanaume milioni 2.6 wanatumia dawa za kuongeza nguvu; ndio nasema kwamba sisi Tanzania hatujafanya utafiti rasmi uliotangazwa na Serikali, lakini wewe bila shaka utakuwa shahidi kwamba ziko dalili kwamba hali ni mbaya.
Kuna mtafiti mmoja maarufu kutoka India, Dk Srini Vasakumar, kutoka kituo cha utafiti wa tiba kiitwacho Institute of Biology and Clinical, India, ambaye amekuwa akitoa huduma za kuponya tatizo hilo la udhaifu katika maeneo mbalimbali hapa nchini, anasema hili ni tatizo linaloweza kupona, shida ya wengi ni kutochukua hatua; wengi wanalia, badala ya kuchukua hatua.
Daktari huyo mwenye Shahada ya pili ya Tiba kwa kutumia vyakula na Shahada ya uzamivu ya tiba kwa ujumla, anasema wengi wanaendelea kuwa na tatizo hili kwa  kutochukua hatua thabiti; wengi wamesoma na wanafahamu kuna aina za vyakula vinasaidia wanga, nguvu, mafuta na vitamini... lakini wanakula ili mradi tumbo lijae.
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi, Janet Bina Kahama, Aprili 10, mwaka  2007 katika kikao cha saba cha Bunge aliuliza swali namba 8 (b); je, Serikali inafahamu ni sababu gani zinasababisha kupungua kwa nguvu za kiume kunakotangazwa sana na waganga wa jadi? Aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Prof. David Mwakyusa alijibu kuwa tatizo hili linasababishwa na mambo mengi, baadhi yao ni lishe duni hasa mboga za majani, kutokula aina mbalimbali za jamii ya karanga, matumizi yasiyofaa ya ulevi kama pombe.
Sababu nyingine ni matumizi ya sigara, dawa za kulevya, dawa zinazotibu baadhi ya magonjwa kama kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya akili na kutopumzika kunakosababishwa na shughuli nyingi za kijamii hivyo kusababisha uchovu. 
Kwa uzoefu wangu kama mtu ambaye nimekuwa nikitoa ushauri kuhusu masuala ya ndoa ni kwamba tatizo hili lina athari kubwa katika ndoa, baadhi ya wanawake sasa hawaangalii uzuri wa mwanaume, wala utajiri  au elimu yake ama tabia, kwanza wanatamani kujua kama mume mtarajiwa ni mume dhaifu au la.
Athari za kuwa dhaifu ni kwamba baadhi ya wanawake unaweza kumpa  mamilioni ya fedha, magari nk lakini unachohonga akaenda kuhongwa mwingine. Unamnunulia gari, unaweza kushangaa  unakutana naye anatembea kwa miguu, gari kapewa kijana atanue nalo.
Ninachotaka kusema ni kwamba kila wanaume kuchukua tahadhari juu ya jambo hili ambalo linaonekana wazi kuwakwaza wanawake wengi kiasi cha baadhi kuamua kuvunja uhusiano. Hata hivyo kama mwenzi wako ana tatizo ni vizuri kuangalia namna ya kulitibu, sio kukimbiana, kwani hakupenda kuwa hivyo.posted by http://thesuperonenews.blogspot.com/

0 comments:

Post a Comment