Friday, October 4, 2013

VIDIC: AJIPA AMPA MATUAMAIN MOYES‘MATAJI YAPO MSIMU HUU!’


VIDIC_ZOEZI

NAHODHA Nemanja Vidic anaamini Manchester United inaweza kugombea Ubingwa wa Ligi ikiwa tu Difensi yao inayovuja itazibwa.

JUMAMOSI STADIUM OF LIGHT NA SUNDERLAND!
Man United, ambao katika Mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu England walichapwa 2-1 na West Bromwich Albion Uwanjani Old Trafford, wapo Nafasi ya 12 baada ya Mechi 6.
-TAKWIMU
-Manchester United wapo Nafasi ya 12 kwenye Ligi.
-Wamefungwa Mechi 3 kati ya 6 za Ligi walizocheza.
-Huu ni mwanzo mbovu kwa Miaka 24 tangu Mwaka 1989/90, Sir Alex Ferguson alipoiongoza Timu na kuambua Pointi 7 katika Mechi 6 kama ilivyo sasa.
Jumamosi Man United wapo Ugenini huko Stadium of Light kucheza na Sunderland isiyokuwa na Meneja baada kutimuliwa Paolo Di Canio.
HIMAYA YA DAVID MOYES-MATOKEO:
-MECHI 10: Ushindi 5 Sare 2 Kufungwa 3
Oktoba 2013
2 Oktoba: Shakhtar Donetsk 1 Man United 1[UCL]
Septemba 2013
28 Septemba: Man United 1 West Brom 2 [BPL]
25 Septemba: Man United 1 Liverpool 0 [COC]
22 Septemba: Man City 4 Man United 1 [BPL]
17 Septemba: Man United 4 Bayer 04 Leverkusen 2 [UCL]
14 Septemba: Man United 2 Crystal Palace 0 [BPL]
28 Septemba: Liverpool 1 Man Utd 0 [BPL]
Agosti 2013
26 Agosti: Man Utd 0 Chelsea 0 [BPL]
17 Agosti: Swansea 1 Man Utd 4 [BPL]
11 Agosti: Man Utd 2 Wigan 0 [Ngao ya Jamii]                             
**UCL=UEFA CHAMPIONS LIGI
**BPL=LIGI KUU ENGLAND
**COC=CAPITAL ONE CUP
Vidic amesema: “Lazima tukubali, hatukuanza vizuri. Hatukuwa tukipata uchezaji tunaotaka na tuwe wakweli tukubali tumefanya makosa. Timu hii inao uwezo mkubwa na tunafanyia kazi vizuri. Mara nyingine matokeo hayaji, mara nyingine uchezaji mzuri haupo. Lakini matumaini yapo. Kitu muhimu ni kujihami vizuri. Tukijihami vizuri, tuna nafasi kubwa ya kutwaa Mataji! ”
Hata hivyo yapo matumaini makubwa kuwa mambo yatabadilika, na kama Meneja wao David Moyes alivyodokeza, tayari washacheza na wapinzani wao wakubwa Man City, Liverpool na Arsenal na sasa ni kutia mkazo Mechi nyingine.
Na Vidic amesema kuwa Mechi ijayo na Sunderland ndio muhimu zaidi.
Kwa Mechi hiyo na Sunderland, Wayne Rooney, ambae aliikosa  Mechi ya Jumatano na Shakhtar Donetsk baada kuumia Mazoezini, atakuwepo.
MOYES==KIMBEMBE KINACHOMNGOJA 
[Saa za Bongo]

OKTOBA
SAA
SIKU
BPL
Sunderland v Man United
19:30
Jumamosi Oktoba 5
BPL
Man United v Southampton
17:00
Jumamosi Oktoba 19
UCL
Man United v Real Sociedad
21:45
Jumatano Oktoba 23
BPL
Man United v Stoke
17:00
Jumamosi Oktoba 26
COC
Man United v Norwich City
22:45
Jumanne Oktoba 29

NOVEMBA


BPL
Fulham v Man United
18:00
Jumamosi Novemba 2
UCL
Real Sociedad v Man United
22:45
Jumanne Novemba 5
BPL
Man United v Arsenal
19:10
Jumapili Novemba 10
BPL
Cardiff v Man United
19:00
Jumapili Novemba 24
UCL
Bayer Leverkusen v Man United
22:45
Jumatano Novemba 27
BPL=LIGI KUU ENGLAND


UCL=UEFA CHAMPIONZ LIGI


COC=CAPITAL ONE CUP

0 comments:

Post a Comment