Sunday, October 13, 2013

MAMA WA MWANDISHI WA ITV / RADIO ONE AUAWA KIKATILI


MWANDISHI wa habari wa ITV na Radio One, Ufoo Saro (pichani) amepigwa risasi ya tumbo na kujeruhiwa vibaya, huku mama yake mzazi akipoteza maisha baada ya kupigwa risasi katika tukio hilo leo alfajiri............................................................................

Mwandishi huyo pamoja na mama yake wamefanyiwa kitendo hicho na kijana anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa Ufoo Saro, aitwaye Mushi ambaye inadaiwa alikuwa nao katika mazungumzo eneo la Kibamba nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam ambapo aliwapiga risasi na yeye kujiua kwa risasi.
Mtuhumiwa aliyefanya kitendo hicho anadaiwa kuwa mfanyakazi wa shirika moja la UN.

0 comments:

Post a Comment