Saturday, September 28, 2013

SPURS, CHELSEA TORRES ALIMWA KADI NYEKUNDU!

Tottenham wametoka Sare Bao 1-1 na Chelsea na kuipiku Arsenal kileleni mwa Ligi Kuu England
Gylfi Sigurdsson ndie alieifungia Spurs Bao katika Kipindi cha Kwanza baada ya ushirikiano mzuri kati ya Christian Eriksen na Roberto Soldado na Mpira kumfikia yeye.

MAGOLI:
Tottenham 1
Sigurdsson Dakika ya 19
Chelsea 1
Terry Dakika ya 65
Chelsea walimwingiza Juan Mata mara Kipindi cha Pili kilipoanza na frikiki yake ndio iliunganishwa na John Terry kwa kichwa na kusawazisha Bao.
MSIMAMO:
NA
TIMU
MECHI
PTS
1
Tottenham
6
13
2
Arsenal
5
12
3
Chelsea
6
11
4
Man. City
5
10
5
Liverpool
5
10
6
Everton
5
9
Chelsea walimaliza Mechi wakiwa Mtu 10 baada ya Fernando Torres kupewa Kadi ya Njano ya pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu zikiwa zimebaki Dakika 10 Mpira kwisha.
Sare hii imewafanya Chelsea wakamate Nafasi ya 3.
Kivutio cha Mechi hii kilikuwa mzozo kati ya Andre Villas-Boas na Jose Mourinho, Watu ambao wanatoka Nchi moja Ureno na walifanya kazi pamoja kwa Miaka 7, waliporushiana maneno lakini kabla ya Mechi kuanza walipeana mikono na mwisho wa Mechi kukumbatiana.
VIKOSI:
Spurs: Lloris, Walker, Dawson, Vertonghen, Naughton, Paulinho, Dembele, Townsend, Eriksen, Sigurdsson, Soldado
Akiba: Chiriches, Lamela, Holtby, Defoe, Chadli, Friedel, Sandro.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Luiz, Terry, Cole, Ramires, Mikel, Lampard, Oscar, Torres, Hazard
Akiba: Essien, Mata, Schurrle, Schwarzer, Cahill, Azpilicueta, Eto'o.
Refa: Mike Dean
RATIBA:
BPL: LIGI KUU ENGLAND
Jumapili 29 Septemba
15:30 Stoke City v Norwich City
18:00 Sunderland v Liverpool
Jumatatu 30 Septemba
22:00 Everton v Newcastle United  
 Posted by Thesuperonews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment