Thursday, September 19, 2013

KAMPENI YA USHOGA: MAN UNITED, SPURS & NORWICH ZAGOMEA!

BUTI-NYUZI_ZA_USHOGA

BAADHI ya Klabu za Ligi Kuu England, zikiwemo Mabingwa Manchester United, Tottenham na Norwich City, zimegoma kutoa sapoti kwenye Kampeni ya Kutetea Haki za Ushoga.

KLABU 29 ZINAZOSAPOTI MASHOGA:
-LIGI KUU ENGLAND: Arsenal, Aston Villa, Crystal Palace, Liverpool, Manchester City, Norwich, Sunderland, West Ham, West Brom
-CHAMPIONSHIP: Birmingham, Blackburn, Doncaster, Huddersfield, Ipswich, Leicester, Millwall, Sheffield Wednesday
-LIGI 1: Carlisle, Crewe, Gillingham, Leyton Orient, MK Dons, Peterborough, Preston, Tranmere
-LIGI 2: Bristol Rovers, Exeter, Dagenham & Redbridge, Northampton
**LISTI IMEHAKIKIWA TAREHE 18 Machi 2013
Hivi Majuzi, Wachezaji wa Soka huko England na Scotland walialikwa kuisaidia Kampeni ya kuunga mkono Mashoga kwa kutakiwa kufunga Nyuzi za Rangi ya ‘Upinde wa Mvua’ kwenye Buti zai wakati wa Mechi za Wikiendi hii na Taasisi ya Hisani ya Mashoga, Stonewall, ilishamsambaza Nyuzi hizo spesho kwa Vilabu 92 vya Ligi Kuu England na Klabu za Ligi za Madaraja ya chini na pia Klabu 42 za Soka ya Kulipwa huko Scotland.
Kwenye Kampeni hii, iitwayo The Right Behind Gay Footballers, Wachezaji wameombwa kutumia Nyuzi hizo kwenye Mechi za Septemba 21 na 22.
Lakini Klabu nyingi zimeonyesha kutoridhishwa kwao kwa jinsi Kampeni hiyo inavyoendeshwa na Taasisi ya Hisani ya Mashoga, Stonewall, na Kampuni ya Kamari, Paddy Powers, bila ya wao kuhusishwa tangu awali.
Tamko rasmi la Mabingwa Manchester United limesema Klabu hiyo haitavaa Nyuzi hizo huku nao Tottenham wakiwa na msimamo huo huo pamoja na Norwich ambao Meneja wao Chris Hughton amesema Wachezaji wake hawatavaa Nyuzi hizo.
Juzi Wasimamizi wa Ligi Kuu England walisema ni juu ya Klabu na Wachezaji kuamua msimamo wao juu ya Kampeni hii.
HABARI ZA AWALI:
LIGI KUU ENGLAND: NI JUU YA KLABU, WACHEZAJI KUAMUA KUVAA NYUZI ZA ‘USHOGA’!!
Wednesday, 18 September 2013 16:35
>>WIKIENDI WACHEZAJI KUVAA BUTI ZENYE NYUZI RANGI ‘UPINDE WA MVUA!’
WASIMAMIZI wa LIGI KUU ENGLAND wamesema ni juu ya Klabu zenyewe na Wachezaji wenyewe kuamua kama wataunga mkono Kampeni ya Kutetea Haki za Mashoga kwa kufunga Nyuzi za Rangi ya ‘Upinde wa Mvua’ kwenye Buti zao wakati wa Mechi za Ligi za Wikiendi hii.
Tayari Taasisi ya Hisani ya Mashoga, Stonewall, imetuma Nyuzi hizo spesho kwa Vilabu 92 vya Ligi Kuu England na Klabu za Ligi za Madaraja ya chini na pia Klabu 42 za Soka ya Kulipwa huko Scotland.
Kwenye Kampeni hii, iitwayo The Right Behind Gay Footballers, Wachezaji wataombwa kutumia Nyuzi hizo kwenye Mechi za Septemba 21 na 22.
Lakini Msemaji wa Ligi Kuu England amesema: “Ujumbe wa msingi wa Kampeni hii ni mzuri na ni kweli sisi na Wadau wetu tumeshirikiana na Serikali kuhakikisha Ajenda yote ya Usawa inaeleweka na tunashiriki. Lakini hatukuhusishwa mapema kwenye Kampeni hii. Hivyo ni juu ya Klabu na Wachezaji wenyewe kuamua kama wanaisapoti.”
+++++++++++++++++++++++
HABARI YA AWALI:
WACHEZAJI ENGLAND, SCOTLAND WAALIKWA KUSAIDIA MASHOGA!!
Monday, 16 September 2013 16:27
>>WIKIENDI WAOMBWA KUVAA BUTI ZENYE NYUZI RANGI ‘UPINDE WA MVUA!’
>>ZIJUE KLABU 29 ZINAZOSAPOTI MASHOGA HUKO ENGLAND!!
WACHEZAJI Soka huko England na Scotland wamealikwa kuisaidia Kampeni ya kuunga mkono Mashoga kwa kutakiwa kufunga Nyuzi za Rangi ya ‘Upinde wa Mvua’ kwenye Buti zai wakati wa Mechi za Wikiendi hii inayokuja.
Tayari Taasisi ya Hisani ya Mashoga, Stonewall, imetuma Nyuzi hizo spesho kwa Vilabu 92 vya Ligi Kuu England na Klabu za Ligi za Madaraja ya chini na pia Klabu 42 za Soka ya Kulipwa huko Scotland.
Kwenye Kampeni hii, iitwayo The Right Behind Gay Footballers, Wachezaji wataombwa kutumia Nyuzi hizo kwenye Mechi za Septemba 21 na 22.
KLABU 29 ZINAZOSAPOTI MASHOGA:
-LIGI KUU ENGLAND: Arsenal, Aston Villa, Crystal Palace, Liverpool, Manchester City, Norwich, Sunderland, West Ham, West Brom
-CHAMPIONSHIP: Birmingham, Blackburn, Doncaster, Huddersfield, Ipswich, Leicester, Millwall, Sheffield Wednesday
-LIGI 1: Carlisle, Crewe, Gillingham, Leyton Orient, MK Dons, Peterborough, Preston, Tranmere
-LIGI 2: Bristol Rovers, Exeter, Dagenham & Redbridge, Northampton
**LISTI IMEHAKIKIWA TAREHE 18 Machi 2013
Huko Uingereza, haki za Mashoga zinalindwa na hata FA ina msimamo wa kukemea Mashoga kubaguliwa.
Kwa sasa hakuna hata Mchezaji mmoja huko Uingereza alieibuka bayana na kukiri yeye ni Shoga.
Mwaka 1990, Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya England ya U-21 pamoja, Justin Fashanu, alikuwa ni Mchezaji wa kwanza wa Kulipwa kutangaza yeye ni Shoga lakini Mwaka 1998, Fashanu alijiua mwenyewe akiwa na Miaka 37.

0 comments:

Post a Comment