Monday, September 23, 2013

ANGALIA PICHA ZAIDI YA 10 ZA MAJANGA YA FIESTA YALIYOTOKEA SHINYANGA NI NOMAA!!!

 Mwanadada Shilole na madensa wake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Kambarage.mkoani Shinyanga.
 Anajiita Mzee wa Mahaba kutoka Manzabay,Cassim Mganga akiwaimbisha mashabiki wake kwa shangwe huku mayowe yakitawala kila kona ya uwanja wa Kambarage usiku huu ndani wakati tamasha la Serengeti fiesta likiendelea kurindima usiku huu.
 Mtoto wa Mama Said a.k.a Chege akiimba kwa hisia jukwaani.
Msanii wa Bongofleva Ney wa Mitego akiwaimbisha mashabiki wake.
 Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoko akiimba jukwaani usiku huu sambamba na madensa wake (hawapo pichani). 
Tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea usiku huu.

Mashabiki wake wanamuita Kinga Zilla kutoka Sala Sala,lakini pia jina la Godzilla limemuongeza umaarufu kwa mashabiki wake kutokana na umahiri wake wa kushusha mistari ya hip hop mikavu mikavu,kama aonekavyo jukwaani akiwaimbisha mashabiki wake ndani ya uwanja wa Kambarage usiku huu.
  Baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga,ambapo tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea kufanyika.
Mwanadada Linah akiimba sambamba na shabiki wake jukwaani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga usiku.
 Baadhi ya Wadau wakubwa na wadhamini wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2013,kutoka kampuni ya Serengeti Breweries,Octavian,Bahati pamoja na mdau wao,wakiwa katika picha ya pozi usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga
 Mwanadada ambaye kwa sasa ameonekana akifanya vyema kwenye jukwaa la Serengeti fiesta 2013,Neylee akiwaimbisha mashaniki wake (hawapo pichani). 
 Anajiita Jita Man kutoka jijini Mwanza akitumbuiza jukwaani usiku huu.

Dj  akiburuza mangoma usiku huu.

 Mwanadada Shilole na madensa wake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Kambarage.mkoani Shinyanga. 
 Masbabiki kibao waliojitokeza kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,usiku wakifuatilia na kushangweka vilivyo mbele ya jukwaa la fiesta.
 mashabiki wakifuatilia
 Kutoka Wanaume TMK,wakiongozwa Mh Temba na Chege kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la Serengeti fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa kambarage mjini Shinyanga.
 Weusi wakitumbuiza jukwaani usiku huu.
                                                     Shabiki akifurahi jamboo.
                Kundi la Wanaume TMK-Halisi likiongozwa na Sir Juma Nature wakilishambulia jukwaa la Serengeti Fiesta ndani ya uwanja wa Kambaraje,mjini Shinyanga.
Posted by Thesuperonenews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment