Wednesday, June 26, 2013

KOMBE LA MABARA: PAULINHO AWA MUKOZI WA BRAZIL

PAULINHO


































KONA ya Dakika ya 86 ya Neymar ilimkuta Kiungo Paulinho aliejitwika kichwani na kuipa Brazil Bao la pili na la ushindi na kutinga Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara walipoifunga Uruguay Bao 2-1 katika Mechi ya Nusu Fainali iliyochezwa Estadio Mineirao, Mjini Belo Horizonte, Nchini Brazil.
Katika Mechi hii iliyoanza kwa mchecheto kwa Timu zote mbili, hasa kwa vile zinajuana fika na zina uhasama wa jadi, Uruguay walipata nafasi safi ya kupata Bao la kuongoza pale Beki wa Brazil David Luiz alipoadhibiwa kwa kucheza faulo ndani ya boksi wakati wa kona kwa Uruguay kupewa Penati katika Dakika ya 14 ambayo Diego Forlan alipiga na Kipa wa Brazil Julio Cesar kuicheza na kuokoa.
MAGOLI:
BRAZIL
-Fred Dakika ya 42
-Paulinho 86
URUGUAY
-Cavani Dakika ya 48
Lakini ilikuwa kazi njema ya Neymar alieshusha pasi ndefu ya Luis Gustavo kifuani akiwa ndani ya boksi na kugonga mpira ulioguswa na Kipa Muslera na kumkuta Fred aliemalizia vizuri na kuweka Bao la kwanza kwa Brazil.
Uwanja mzima ulishangilia sana Bao hili hasa kwa vile Fred ni ‘Mtoto wa Nyumbani’ hapo Estadio Mineirao.
Uruguay walisawazisha Kipindi cha Pili Dakika ya 48 baada ya makosa ya Mabeki wa Brazil Thiago Silva aliemuuza Marcelo na Edinson Cavani kuunasa mpira na kufunga.
Wenyeji Brazil hawakuvunjika moyo na waliendelea kusakata kabumbu na Uruguay kusimama imara hadi Dakika ya 86 ushindi ulipopatikana.
Kwenye Fainali Jumapili Brazil watacheza na Mshindi wa Nusu Fainali nyingine itakayocheza Alhamisi Usiku kati ya Spain na Italy.
VIKOSI:
BRAZIL: Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz, Marcelo, Oscar, Gustavo, Paulinho, Fred, Hulk, Neymar
Akiba: Jefferson, Fernando, Lucas Moura, Hernanes, Dante, Filipe Luis, Jean, Rever, Bernard, Jo, Jadson, Cavalieri.
URUGUAY: Muslera, Lugano, Godin, Caceres, Maxi Pereira, Rodriguez, Arevalo Rios, Gonzalez, Forlan, Suarez, Cavani
Akiba: Castillo, Coates, Gargano, Pereira, Eguren, Hernandez, Aguirregaray, Lodeiro, Perez, Ramirez, Silva.
Refa: Enrique Osses (Chile)
RATIBA/MATIBA:
NUSU FAINALI
BRAZIL-BIG_SAM_N_PLAYERSJumatano Juni 26
Brazil 2 Uruguay 1
Alhamisi Juni 27
[Fortaleza]
[SAA 4 USIKU]
Spain v Italy
MSHINDI WA TATU
Jumapili Juni 30
[Salvador]
[SAA 1 USIKU]
FAINALI
Jumapili Juni 30
[Rio De Janeiro]
[SAA 7 USIKU]

0 comments:

Post a Comment