Thursday, June 27, 2013

KOMBE LA MABARA: LEO NUSU FAINALI SPAIN YAAPA KUFANYA MAUAJI


SPAIN_v_ITALY
LEO USIKU, Nusu Fainali ya pili ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara inachezwa huko Estadio Castelao, Mjini Fortaleza Nchini Brazil kati ya Mabingwa wa Dunia Spain na Italy kutafuta mpinzani wa Brazil ambao jana walitinga Fainali baada ya kuifunga Uruguay Bao 2-1.

Kocha wa Spain Vicente Del Bosque inabidi asubiri Madaktari wa Timu waamue kama Wachezaji Fabregas na Soldado, ambao wanakabiliwa na matatizo ya Musuli, wako fiti kucheza Mechi na Italy.
Nao Italy ndio wameathirika sana na majeruhi baada ya Wachezaji wao wawili kurudishwa Nyumbani baada ya kuumia na alitangulia Fulbeki Abate na Juzi kufuatia Straika Mario Balotelli.
Pia, Kiungo Mkongwe Andrea Pirlo aliikosa Mechi na Brazil Jumamosi iliyopita kwa kuwa na maumivu lakini leo anatarajiwa kucheza pamoja na Montolivo ambae alikuwa kaumia.
Vile vile Kiungo Daniele De Rossi anaweza kucheza Mechi hii baada ya kuikosa ile na Brazil baada ya kuwa kwenye Kifungo cha Mechi moja.
Timu zote, Spain na Italy, hazina Mchezaji alie Kifungoni.FIFA_CONFEDERATION_CUP_BRAZIL_2013
Tathmini ya Mechi
Spain wanatoka kwenye ushindi mnono baada ya kuitwanga Nigeria 3-0 katika Mechi yao ya mwisho ya Kundi B na kumaliza hatua hiyo wakionyesha wana Difensi nzuri na Fowadi hatari katika Mashindano haya.
Kitu kingine cha faida kwa Spain ni kuwa Straika wao Fernando Torres ameonyesha yuko imara baada ya kufunga Bao 5, 4 dhidi ya Tahiti walipoibamiza 10-0 na moja dhidi ya Nigeria, na hilo linatia moyo kuwa atamudu kucheza vyema ikiwa Soldado, ambae ndie kawaida huanza Mechi, atashindwa kucheza.
Italy wanatoka kwenye kipigo cha Bao 4-2 toka kwa Brazil lakini walicheza Mechi hiyo bila nguzo zao imara kwenye Kiungo kwa kuwakosa Pirlo na De Rossi.
Lakini pia wataingia kwenye Mechi bila ya Straika wao Balotelli na hivyo watalazimika kumchezesha Gilardino au El Shaarawy kama Straika pekee kwa mujibu wa Mfumo wao wa 3-4-2-1.
Uso kwa Uso
Tangu Mwaka 1924, Spain na Italy zimekutana mara 27 na kila Timu imeshinda mara 8 na Sare 1.
Mara za mwisho kukutana ni kwenye EURO 2012 ambako walikuwa Kundi moja na kutoka Sare Bao 1-1 na kisha kukutana tena kwenye Fainali na Spain kushinda Bao 4-0 kwa Bao za Silva, Alba, Torres na Mata.
VIKOSI VONATARAJIWA:
SPAIN [Mfumo: 4-3-3]:
Casillas
Arbeloa-Ramos-Piqué-Alba
Xavi-Busquets-Iniesta
Pedro-Torres-Silva
ITALY [Mfumo: 3-4-2-1]:
Buffon
Barzagli-Chiellini -Bonucci
Maggio-Pirlo-Rossi -Giaccherini
Candreva-Marchisio
Gilardino
REFA: Howard Webb [England]
RATIBA/MATOKEO:
NUSU FAINALI
Jumatano Juni 26
Brazil 2 Uruguay 1
Alhamisi Juni 27
[Fortaleza]
[SAA 4 USIKU]
Spain v Italy
MSHINDI WA TATU
Jumapili Juni 30
[Salvador]
[SAA 1 USIKU]
FAINALI
Jumapili Juni 30
[Rio De Janeiro]
[SAA 7 USIKU]
Brazil v Spain/Italy

0 comments:

Post a Comment