Monday, June 24, 2013

TAARIFA TOKA TFF:MCHEZAJI WA ZAMANI WA TAIFA STARS AAGA DUNIA

TFF_LOGO12
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Cosmopolitan na Taifa Stars, Mathias Kissa (84) kilichotokea leo alfajiri (Juni 24 mwaka huu) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani enzi zake, Kissa akiwa na timu ya Tabora alitamba katika michuano ya Kombe la Taifa wakati huo ikiitwa Sunlight Cup. Alikuwa akicheza katika nafasi ya ulinzi.
Baadaye alijiunga na Cosmoplitan ya Dar es Salaam, na pia kuwa mchezaji wa timu ya Taifa ambapo enzi zake akiwa na wachezaji kama Yunge Mwanansali wakiiwakilisha Tanganyika na baadaye Tanzania Bara walitamba katika michuano ya Kombe la Chalenji wakati huo ikiitwa Gossage, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Kissa ambaye alipata tuzo ya mchezaji bora wa karne kwa upande wa Tanzania, tuzo inayotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) alikuwa ndiye mchezaji msomi kupita wote wakati akichezea timu ya Taifa akiwa amehitimu elimu ya Darasa la Kumi.
Kwa mujibu wa binti yake, Erica, marehemu ambaye pia aliwahi kuwa mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi (stroke) alioupata miaka mitano iliyopita, na kisukari. Baadaye alipata kidonda ambacho ndicho kilichosababisha kifo chake.
Msiba uko nyumbani kwa marahemu, Masaki, Mtaa wa Ruvu karibu na Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST). Maziko yatafanyika keshokutwa, Jumatano (Juni 26 mwaka huu) kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kisa, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na klabu ya Cosmopolitan na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Kisa mahali pema peponi. Amina
KIUNGO wa Simba, Amri Kiemba, ndie lietwaa Tuzo ya Mchezaji Bora kwa Msimu uliopita iliyotolewa na Soccer Players' Union of Tanzania (SPUTANZA) katika Tamasha maalum lililofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam Jumamosi Usiku.
Hili ndio Tamasha la kwanza kwa SPUTANZA kuandaa na kutoa Tuzo za aina hii.
Kiemba alizoa Asilimia 47.88 ya Kura zilizopigwa na Makocha na Manahodha wa Klabu za LigI Kuu Vodacom.
Ni Makocha na Manahodha 17 kati ya 28 ndio waliohudhuria Tamasha hilo wakati ilitarajiwa watakuwepo Kocha na Nahodha wake kwa kila Timu toka Klabu 14 za Ligi Kuu Vodacom.
Katika uchaguzi wake, Kiemba aliwabwaga Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu na Paul Nonga.
Kwenye Tuzo ya Mchezaji Kijana Bora, Kiungo wa Azam FC Salum Abubakar aliwabwaga Shomari Kapombe (Simba), Issa Rashid (Mtibwa) na Hassan Dilunga (JKT Ruvu).
Mshindi wa Kipa Bora alikuwa ni Kipa wa Mtibwa Sugar, Hussen Shariff, aliewashinda Kipa wa Simba Juma Kaseja na Mwadini Ally wa Azam FC.
Nae Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, alitwaa Tuzo ya Kocha Bora kwa kumshinda Abdallah Kibaden ambae alikuwa Kocha wa Kagera Sugar ingawa sasa yuko Simba pamoja na Jumanne Chale.
Akiongelea uteuzi wa Wagombea Tuzo hizo, Katibu wa SPUTANZA, Said George, alisema wao walitumia Takwimu walizopewa na TFF, Shirikisho la Soka Tanzania na pia alielezea kuridhika kwao na uendeshwaji na mafanikio ya Tamasha lao hilo la kwanza na kuahidi kuliboresha zaidi kwa Msimu ujao.posted by www,Thesuperonenews.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment