Friday, June 7, 2013

AFRIKA NA KOMBE LA DUNIA WIKIENDI HII NCHI 3 ZINAWEZA KUSONGA


MBWANA_SAMATA12HUKU kukiwa na Mechi 3 zilizobaki kwenye hatua ya Makundi ya kutafuta Nchi 10NGASSA zitakazoingia hatua ya mwisho ya Mtoano ya kupata Nchi 5 zitakazotinga Brazil Mwaka 2014 kwenye Fainali za Kombe la Dunia, Tunisia, Egypt na Congo, Timu pekee zilizoshinda Mechi zao zote 3 za kwanza, zina nafasi kusonga Wikiendi hii ikiwa watashinda Mechi zao na matokeo mengine kuwasaidia huku Nchi yetu, Tanzania, ambayo bado ipo sana kwenye kinyang’anyiro, ikiwa ugenini kucheza na Morocco.
MUNGU IBARIKI  AFRIKA LAKINI PIA IBARIKI TANZANIA!
Tanzania, wakiwa KUNDI C, wapo Nafasi ya Pili Pointi 1 moja nyuma ya Vinara Ivory Coast na matokeo mazuri kwao dhidi ya Morocco ni muhimu ikiwa wanataka kuipiku Ivory Coast ambayo itakuwa Ugenini kucheza na Gambia.
KUNDI C
Ivory Coast Pointi 7
Tanzania 6
Morocco 2
Gambia 1
Kwenye KUNDI E, Congo wapo Ugenini kucheza na Gabon na wao, ambao ni Vinara kwa Pointi 6, watafuzu wakishinda na pia Mechi nyingine kati ya Niger na Burkina Faso ikimalizika sare.
Nao Egypt, Vinara wa KUNDI G, wataingia Raundi ya Mwisho wakishinda Mechi yao ya Ugenini na Zimbabwe na wakati huo huo Mozambique kutoka Sare Ugenini na Guinea.
Tunisia, ambao wako KUNDI B, watafuzu wakiifunga Sierra Leone Ugenini na wakati huo huo Equatorial Guinea wakishindwa kuifunga Cape Verde Islands.
ETOO_CAMEROUNKwenye KUNDI D, Zambia wanaongoza kwa Pointi 1 mbele ya Ghana, Jumamosi wako Nyumbani kucheza na Lesotho na Ghana wana Mechi ngumu Ijumaa Usiku Ugenini huko Khartoum kuivaa Sudan.
Cameroon, chini ya Kocha mpya Volker Finke, wako Ugenini kucheza na Togo wakisaka kuendeleza uongozi wao KUNDI I wa Pointi 1 dhidi ya Libya ambao Ijumaa Usiku wako Nyumbani kucheza na Congo DR, hii ikiwa Mechi yao ya kwanza kucheza Nchini kwao katika Miaka miwili.
Cameroon watacheza Mechi yao bila ya Staa wao Samuel Eto'o ambae aliumia akiiwakilisha Klabu yake Anzhi Makhachkala kwenye Fainali ya Kombe la Russia.
Mechi za Raundi ya 4 ya Hatua ya Makundi za KUNDI F zilichezwa mapema Jumatano kwa vile Nigeria wanahitajika kuliwakilisha Bara la Afrika kama Mabingwa wao huko Brazil kwenye Mashindano ya Fifa ya kombe la mabara  yanayoanza Juni 15.
RATIBA/MATOKEO:
Jumatano Juni 5
Kenya 0-1 Nigeria
Malawi 0-0 Namibia
Ijumaa Juni 7
18:30 Libya v Congo, DR
20:00 Sudan v Ghana
Jumamosi Juni 8
16:00 Uganda v Liberia
16:00 Zambia v Lesotho
16:00 Botswana v Ethiopia
17:00 Central African Republic v South Africa
17:30 Gabon v Congo
18:00 Angola v Senegal
19:30 Gambia v Ivory Coast
19:30 Sierra Leone v Tunisia
20:30 Cape Verde v Equatorial Guinea
23:00 Morocco v Tanzania
Jumamosi Juni 8
Niger v Burkina Faso
Zimbabwe v Egypt
Guinea v Mozambique
Benin v Algeria
Mali v Rwanda
Togo v Cameroon
RAUNDI YA PILI
[Kila Timu imecheza Mechi 3 isipokuwa inapotajwa]
KUNDI A
Ethiopia Pointi 7
South Africa 5
CAR 3
Botswana 1
KUNDI B
Tunisia Pointi 9
Sierra Leone 4
Eq Guinea 4
Cape Verde 0
KUNDI C
Ivory Coast Pointi 7
Tanzania 6
Morocco 2
Gambia 1
KUNDI D
Zambia Pointi 7
Ghana 6
Lesotho 2
Sudan 1
KUNDI E
Congo Pointi 9
Burkina Faso 3
Niger  3
Gabon 3
KUNDI F
[Kila Timu imecheza Mechi 4]
Nigeria Pointi 8
Malawi 6
Namibia 4
Kenya 2
KUNDI G
Egypt Pointi 9
Guinea 4
Mozambique  2
Zimbabwe 1
KUNDI H
Algeria Pointi 6
Mali 6
Benin 4
Rwanda 1
KUNDI I
Cameroon Pointi 6
Libya 5
Congo DR 4
Togo 1
KUNDI J
Senegal Pointi 5
Liberia 4
Angola 3
Uganda 2

0 comments:

Post a Comment