Wednesday, June 5, 2013

DENI WARILOLILIMBIZA TFF LAANZA KUWATOKEA PUAN TARATIBU WAANZA NA BASI LA TFF LILO PIGWA TAPLO KUTOKANA NA DENI WANALODAIWA

Magari binafsi ya maofisa wa TFF wa TFF yakwia getini






Shirikisho  la Soka Tanzania (TFF) leo limejikuta likipata aibu ya mwaka baada ya Kampuni ya Flamingo Auction Mart, kuyapiga tanganyika jeki mabasi ya shirikisho hilo kutokana na deni la zaidi ya Sh.50 milioni wanalodaiwa na Kampuni ya Safina Holding ya jijini Dar es Saalam. 

Kampuni hiyo ya Flamingo  ilitia timu kwenye ofisi za shirikisho hilo kufuatia amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni ikitaka zoezi la ukamataji magari hayo hadi Juni 30 liwe limeshakamilika.
Fedha hizo za Safina Holding zimetokana na hifadhi ya baadhi ya timu zilizoshiriki michuano ya Kombe la Kagame mwaka jana na Yanga kuibuka kidedea. Magari ambayo yameamriwa na mahakama hiyo kukamatwa ni basi aina ya Yutong lenye namba za usajili T 581 CGR amoja na Toyota Mini Bus lenye namba za usajili T 528 ASJ. 
Lakini tofauti na amri hiyo ya Mahakama maofisa hao wa Flamingo walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuingia kwenye mzozo na maofisa wa TFF na kuzuka zogo kubwa huku maofisa hao wa TFF kuzuia magari hayo yasichukuliwe.
Maofisa hao wa Flamingo wakiongozwa na Meneja Operation wao Noel Nyalila walitinga kwenye ofisi hizo na kulifunga gari lenye namba za usajili T 528 ASJ aina ya Coster na kulivuta kwenye gari lao lenye namba T 972 ABJ Jay Ambe, lakini walishindwa kuondoka nalo baada maofisa wa
Angetile Osiah akionesha barua yenye utata
TFF  kuzuia kwenye geti. 
 Wafanyakazi hao wa TFF waliamua kuzuia kwa kuegesha magari yao binafsi getini. Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osia alisema waliamua kufanya hivyo baada ya barua ya  Mahakama alidai kuwa inaonyesha kwamba amri hiyo inapaswa kutekelezwa Juni 31 mwaka huu. 
 “ Tumelazimika kuzuia kwa sababu mwanasheria wetu amekwenda mahakamani ili kupata udhibitisho wa amri hii, kwa sababu tarehe ya kukamata magari haya ambayo ni Coster yenye namba T 528 ASJ na basi lenye namba T 581 CGR ni kweli tunadaiwa lakini tuna mpango wa kulipa,” alisema Osiah. 
Kwa upande wake Meneja Noel alisisitiza kwamba amri hiyo ni halali na wamefika hapo ili kuitekeleza kwa kuwa hukumu ilitolewa April 23 mwaka huu, amri ikaandikwa Juni 3 mwaka huu, ambapo June 31 wanapaswa kurejea mahakamani. Hata hivyo waliomba msaada wa Polisi ili waweze kusimamia kuyachukua magari hayo, na kufanikiwa
Basi la TFF likipigwa Tanganyika jeki



0 comments:

Post a Comment