skip to main |
skip to sidebar
BARCELONA BAADA YA KUMALIZA LIGIYA LALIGA WAMEFANIKIWA KUVUNJA REKODI YA MOURINHO NA PEP GUARDIOLA
Mabingwa wa La Liga Barcelona baada ya kubeba ubingwa wa laliga
wamefanikiwa kuifikia rekodi ya pointi nyingi zaidi kwenye ligi hiyo kwa
kumaliza ligi na jumla ya pointi 100 - pia wakaweka rekodi ya kufunga
mabao mengi zaidi - magoli 115 baada ya kuichabanga
Malaga 4-1 kwenye mchezo wa mwisho wa La Liga.
Kwenye msimu wake wa kwanza kocha Tito
Vilanova ameweza kuifikia rekodi ya Jose Mourinho alipoiongoza Real Madrid
kumaliza ligi na pointi 100, pia ameweza kuivunja rekodi ya Pep
Guardiola aliyeiongoza Barca kuweka rekodi ya kufunga mabao 114 msimu
uliopita.
Barca walimaliza ligi na ubingwa
wakiweza kufunga katika kila mechi ya ligi(38) na wamewazidi Real
Madrid walioshika nafasi ya pili kwa mabao 15.
0 comments:
Post a Comment